Hivyo basi, Manabii عَـلَيْـهِمُ الـصَّلٰوة ُ وَالـسَّلَام na watu wema رَحِمَهُمُ الـلّٰـهُ تَـعَالٰی wapo hai na sisi hatuombi msaada kutoka kwa wafu bali tunaomba msaada kutoka kwa wale walioko hai tu. Nasi tunaamini kuwa wao ni wasaidizi kwa idhini yake Allah عَزَّوَجَلَّ na bila ya idhini yake mtume yoyote wala mcha Mungu hawezi kutupatia sisi aina yoyote ile ya msaada.
Imamu wa mamilioni ya wafuasi wa madhehebu ya kihanafi Imam al-A'zam Abu Hanifa رَحْمَةُ اللهِ تَعَالٰی عَلَيْه Ameomba msaada kwa Mtume صَلَّى اللهُ تَعَالٰى عَلَيْهِ وَاٰلِهٖ وَسَلَّم katika Qasid-e-Un’man:
جُدۡلِيۡ بِجُوۡدِكَ وَ اَرۡضِنِيۡ بِرِضَاكَ |
يَا اَكۡرَمَ الثَّقَلَيۡنِ يَا كَنۡزَ الۡوَرٰي |
لِاَبِيۡ حَنِيۡفَةَ فِي الۡاَنَامِ سِوَاكَ |
اَنَا طَامِعٌ بِالۡجُوۡدِ مِنۡكَ لَمۡ يَكُنۡ |
Ewe mbora kuliko binadamu wote na majini! Ewe hazina ya Allah عَزَّوَجَلَّ nakuomba unipe kwa ukarimu wako na uniridhishe kwa kuniridhia. Mimi nataraji ukarimu wako. Hakuna msaidizi kwa Abu Hanifa رَحْمَةُ اللهِ تَعَالٰی عَلَيْه katika watu isipokuwa wewe.
صَلُّوۡا عَلَى الۡحَبِيۡب صَلَّى اللّٰهُ تَعَالٰى عَلٰى مُحَمَّد
Sheikh Imam Sharaf-ud-Din Būsirī عَـلَيْهِ رَحْـمَةُ الْـمَنَّانْ ameomba